Kishore Kumar Hits

Adawnage - Tulizo lyrics

Artist: Adawnage

album: Maisha


Kwa kweli ulinipenda nikiwa bado sijakujua
Ukanipa mwanga wako nisije kwamba nikateleza
Ukaniita mwana wako, vidonda vyote ukaviziba
Na sasa niko huru, lawama yote ulijitwika
Ni wewe tu, muumba vyote ulinipenda
Ni wewe tu, maisha yangu kafanya mapya
Ni wewe tu, tulizo wa moyo wangu
Ni wewe, ni wewe ni wewe
Nauliza, nimuishie nani mimi
Nauliza, nimuabudu nani mimi
Jehovah nimenyosha mikono, nitakuabudu milele
Muweza, unaweza, na hakuna kama wewe
Nauliza, nimkimbilie nani mimi?
Nauliza, nimuogope nani mimi?
Masiya, hakuna haya ya kukimbilia wewe
Kwa maana nimeona hakuna kama wewe
(Refrain)
Hakuna, hakuna, mwenye penzi kama lako Baba
Hakuna, hakuna, baraka kama zako wewe
Hakuna, hakuna, aliyenifia ila wewe
Hakuna, hakuna, ee ee
(Refrain)

Поcмотреть все песни артиста

Other albums by the artist

Similar artists