Kishore Kumar Hits

Rebekah Dawn - Hatua Kwa Hatua lyrics

Artist: Rebekah Dawn

album: This Chosen Road


Sauti nyingi zinanizingira
Mawaitha mingi, njia nyingi
Lakini najua Sauti moja tu la kufuata
Sina Mchungaji mwingine ila Yesu
Hata wengine wakiteleza njiani
Nitazidi kuwa mwaminifu Kwake
Nitaamini neno Lake
Hajawahi kunipotosha
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Oooh, Nitaendelea
Njia zake zaaminika
Neno lake ni la kweli
Kwa hilo nitasimama
Sitainamia dunia
Sina Mwongozo mwingine ila Yesu
Sijawahi ona mwenye haki ameachwa
Waliokuchagua hawajawahi kujuta
Kwa hivyo nitazidii Nawe, hata nisipoelewa
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Nitakufuata Yesu

Nitakufuata Yesu, Kiongozi mwema
Mkombozi, sina mwingine
Mfalme, sina mwingine
Mwenye Enzi, sina mwingine
Msaidizi, sina mwingine
Mponyaji, sina mwingine
Mtetezi, sina mwingine
Mwokozi, sina mwingine
Mfariji, sina mwingine
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Nitaendelea, Ooooh

Nitaendelea na Wewe, Yesu
Mkombozi, sina mwingine
Mfalme, sina mwingine
Mwenye Enzi, sina mwingine
Msaidizi, sina mwingine
Mponyaji, sina mwingine
Mtetezi, sina mwingine
Mwokozi, sina mwingine
Mfariji, sina mwingine
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Поcмотреть все песни артиста

Other albums by the artist

Similar artists